Jumanne 18 Novemba 2025 - 17:23
Istanbul yaandaa kumbukizi ya Allamah Tabataba’i (ra)

Hawza/ Katika semina iliyoandaliwa kutokana na juhudi za “Aka­d­emi ya Kawthar”, mtafiti na mwandishi kutoka Uturuki, Bwana Musa Güneş, alitoa muhadhara na kuchambua nafasi na mchango wa Allamah Sayyid Muhammad Husayn Tabataba’i (ra) katika nyanja za tafsiri, falsafa na irfani.

Kwa mujibu wa Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Habari la Hawza kutoka Istanbul, sambamba na kukumbuka mwaka wa arobaini na nne tangia kufariki kwa Allamah Sayyid Muhammad Husayn Tabataba’i, semina yenye anuani isemayo “Nafasi na mafanikio ya kielimu ya Allamah Tabataba’i katika fikra ya Kiislamu ya kisasa” iliandaliwa Jumamosi, tarehe 15 November 2025 katika Kituo cha Utamaduni cha Kawthar.
Lengo la semina hii lilikuwa ni kusoma upya urithi wa fikra za Allamah na kuchunguza ufanisi wa kazi zake katika kukabiliana na masuala ya leo ya ulimwengu wa Kiislamu.

Ufunguzi wa semina: Kusomwa Qur’ani na Risala fu ya maisha yake

Semina ilianza kwa kisomo cha aya za Qur’ani Tukufu. Baada ya hapo, video ya makala ya kimaandishi iliyoonesha maisha, shughuli za kielimu na kazi za Allamah Tabataba’i ilioneshwa.
Katika makala hiyo, hasa ilisisitizwa juu ya tafsiri yake “al-Mizan” na vipengele vya kimawazo na kijamii vya mtazamo wake wa kifalsafa–kisirafani.

Hotuba ya ufunguzi

Yusuf Tazegün, katika hotuba yake ya ufunguzi, alieleza kuwa lengo la Akademi ya Kawthar katika kuandaa programu kama hizi ni “kuhamisha urithi wa kielimu kwa vizazi vijavyo na kuunganisha maandishi ya kale na fikra za kisasa.”
Alisisitiza kuwa kazi za Allamah Tabataba’i sio urithi wa kitaaluma tu, bali ni mwongozo wa fikra na mwenendo kwa msomi Mwislamu wa leo.

Hotuba kuu

Katika sehemu kuu ya semina, Musa Güneş alifafanua mtazamo wa kimaudhui na kimetodolojia wa Allamah Tabataba’i. Miongoni mwa mambo aliyoyaelezea ilikuwa ni: Kuchanganya akili, riwaya, uchambuzi wa kifalsafa na shuhudi ya kiirfani katika mbinu ya Allamah, mtazamo wake wa kimaeneo mengi katika kusoma Qur’ani: kihistoria, kilugha na kimetafizikia, na nafasi ya mtazamo huu katika kuimarisha uelewa wa fikra ya Kiislamu ya kisasa.

Güneş, kwa kutoa mifano kutoka katika uchambuzi wa “al-Mizan”, alionesha kuwa baadhi ya tafsiri za Allamah zina uhusiano wa moja kwa moja na masuala ya kimaadili, kisiasa na kijamii ya leo, na zinaweza kutumiwa na watafiti wa teolojia, wanasheria, wanafalsafa na watafiti wa sayansi jamii. Aidha, alirejea uhusiano wa fikra za Allamah na urithi wa Mulla Sadra pamoja na ubunifu wake katika mantiki ya kuwepo na elimu.

Mazungumzo na ushiriki wa watafiti vijana

Moja ya vipengele muhimu vya semina ilikuwa ni ushiriki hai wa washiriki, hasa watafiti vijana. Maswali yaliulizwa kuhusu matumizi ya mbinu ya Allamah katika masuala ya kisasa na pia umuhimu wa kutafsiri na kuzieneza kimataifa kazi zake. Musa Güneş alisisitiza kuwa mwelekeo kama huu unaweza kufungua milango ya tafiti za taaluma mseto na kuimarisha uzalishaji wa kielimu.

Mwisho wa programu na taarifa kuhusu mipango ijayo

Mwisho wa semina, waandaaji waliwashuku wahudhuriaji na walitangaza kuwa programu hii ni sehemu ya mfululizo wa vikao vya kielimu vya Akademi ya Kawthar ambavyo vitaendelea katika miezi ijayo.
Viongozi wa Akademi ya Kawthar pia walitangaza mipango ya kutafsiri kazi za Allamah, kuanzisha warsha, na kukuza miradi ya taaluma mseto ili kuutambulisha ipasavyo na kwa upana zaidi urithi wa fikra za Allamah Tabataba’i.

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha